Quantcast
Channel: Kijiwe chetu blog
Viewing all articles
Browse latest Browse all 1649

PUMZIKA KWA AMANI COMRADE JULIUS KAMBARAGE NYERERE.

$
0
0
Tarehe kama ya leo miaka kumi na tano iliyopita giza nene na wingu zito vilitanda juu ya ardhi ya Tanzania na Africa kwa ujumla. Mshangao mkuu na mduwao mkuu ulijaa ndani ya vichwa vya watanzania. Tabasamu na vicheko vilivyodumu ndani ya nyuso za watanzania vilitoweka na kurithiwa na vilio machozi na maombolezo kila kona. 

Hivi vyote vilitokana na Rais wa jamhuri wa Tanzania kuutangazia ulimwengu kuwa, mwana wa Afrika, kipenzi cha waafrika, mzalendo na mwana majumui wa Kiafrika hashirikiani nasi tena kutumia pumzi aliyotupa Mwenyezi Mungu. Hakika vyema havidumu, mwl. Haupo nasi tena duniani kimwili ila jina lako linaendelea kuishi kwa wema na haki duniani.

Taswira mbalimbali za Mwalimu Julius Kambarage Nyerere enzi za uhai wake

Mwalimu akisalimiana na Rais Iddi Amini Dadah wa Uganda wakati wa kikao cha OAU mjini Addis Ababa, Ethiopia enzi hizo. Kushoto kwa Mwalimu ni Waziri wa Mambo ya Nje Mhe John Malecela
Mwalimu akiwa na mume wa Malkia wa Uingereza, Prince Philip
Mwalimu akimlaki Waziri Mkuu wa wa Kwanza wa China Chou Enlai ambaye mtindo wake wa mashati ilirithiwa na Watanzania na kujulikana kama Chunlai
Mwalimu katika mazungumzo na Rais Iddi Amin Dadah wa Uganda. Kushoto ni Mama Maria Nyerere
Mwalimu Nyerere alkiongoza matembezi ya kuunga mkono Azimio la Arush
Familia ya Mwalimu Nyerere
Picha rasmi ya Mwalimu na Mama Maria Nyerere
Mwalimu na Madiba
Mwalimu na Mhe John Samwel Malecela
Mwalimu akimkumbatia Jakaya Mrisho Kikwete baada ya kutoa hotuba ya kukubali matokeo ya Urais alipogombea kwa mara ya kwanza mwaka 2005. Mhe Benjamin Mkapa alishinda
Mwalimu  na Mama Maria Nyerere











































































Viewing all articles
Browse latest Browse all 1649

Trending Articles