Quantcast
Channel: Kijiwe chetu blog
Viewing all articles
Browse latest Browse all 1649

CHADEMA YAIBURUZA CCM KILIMANJARO

$
0
0
MGOMBEA wa Udiwani kata ya Kiboriloni kwa tiketi ya Chadema,Frank Kagoma ameibuka Mshindi katika uchaguzi huo uliuohusisha vyama vitatu, Chadema, CCM na UDP.

akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, Msimazi wa Uchaguzi, Shaban Ntarambe alisema uchaguzi huo ulikuwa huru na haki ambapo kutokana na kura zote zilizopigwa 1288, Kagoma ambaye ni Mwenyekiti wa kata ya Mnazi alipata kura 1019 dhidi ya kura 255 alizopata mpinzani wake wa karibu mgombea wa CCm, Willy Aidano.

Mgombea mwengine, Aidan Muganga Mnzava alijipatia kura 2 ambapo jumla ya kura halali zilikuwa ni 1276 na zilizoharibika ni 12.

Kulikuwa na vituo vikuu vitatu vya kupiga kura pamoja na vingine vidogo 11 na kufanya jumla ya vituo kuwa 14.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 1649

Trending Articles